MMMM TAZAMA HAPA OMMY DIMPOZ NA WEMA SEPETU WALIVYOTUPIA HAPA KI NYAMWENZI

0 comments


Wema  Akiwa  na  SHEMEJI  yake  ndani  ya  pozi  matata
 

HABARI KAMILI ...»

MASKINI ROSE MUHANDO..WAHUNI WAMFANYIA KITU MBAYA MPAKA ANAJUTA SASA

0 comments


MWIMBAJI mahiri wa muziki wa Injili, Rose Muhando amelalamika kuwa albamu yake ya Kamata Pindo la Yesu Albamu anayotarajia kuizindua Jumapili wiki hii imeingizwa mtaani na wezi wa kazi za wasanii, hivyo kuonya wananchi wawe makini kwani albamu yake halisi itatoka Jumapili.
Taarifa kwa vyombo vya habari aliyoitoa Muhando jana, ilieleza kuwa albamu yake halisi bado haijaingia mtaani na kwamba hiyo wanayoiona wananchi sasa ni bandia na mtu atakayewauzia wamripoti polisi. 
“Albamu ya Kamata Pindo la Yesu itaanza kuingia mtaani baada ya uzinduzi wangu kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jumapili wiki hii. Albamu yangu ina nembo ya TRA (Mamlaka ya Kodi ya Mapato nchini). 
 
“Hizi CD zinazouzwa hivi sasa si zangu, hao ni matapeli na nawaomba wananchi tushirikiane kudhibiti wizi. Hao ni maharamia wa kazi za wasanii wanataka kunyonyajasho langu, naomba sana wananchi mnisaidie. 
 
“Nasisitiza albamu yangu sijaiachia sokoni bado mpaka uzinduzi ukamilike, Watanzania wenzangu na mashabiki wangu kote duniani mnielewe na naomba tusaidiane katika hili maana CD feki zimezagaa,” alisema Muhando na kuongez akuwa tayari ameripoti taarifa hiyo kwa vyombo vya dola. 
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions inayoratibu uzinduzi huo, Alex msama naye katika taarifa hiyo ya pamoja alionya wote watakaobanika kuwa CD za albamu ya Rose Muhando watakumbana na mkono wa sheria. 
 
“Inasikitisha sana kuona baadhi ya watu wanataka kutumia jasho la wengine kujinufaisha. Watanzania kuweni macho, msubiri albamu yenyewe ya Rose Muhando Jumapili pale ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam,” alisema Msama. 
 
Albamu hiyo ya Muhando itakayozinduliwa Jumapili ina nyimbo za Bwana Niongoze, Wewe Waweza, Usiniache, Nibariki, Muongo, Kwema, Kamata Pindo la Yesu na Facebook. 
 
Hivi sasa Rose anatamba na albamu yake ya Utamu wa Yesu, ambapo pia amewahi kutamba na albamu za Uwe Macho, Nyota ya Ajabu (Zawadi ya Krismasi), Jipange Sawasawa, Kitimutimu, Mungu Anacheka na Wololo.

HABARI KAMILI ...»

SIRI NJE NJE KUHUSU UGOMVI WA WEMA SEPETU NA MAMA YAKE

0 comments
STAA wa filamu Bongo, Wema Sepetu ametaja sababu zinazomfanya aingie katika mgogoro na mama yake mzazi, Miriam Sepetu kuwa ni suala la uchumba wake na Nasibu Abdul ‘Diamond’ ambao alikuwa akiupinga mara kwa mara.

Staa wa filamu Bongo, Wema Sepetu.
Akipiga stori na mapaparazi, Wema alisema kwa muda mrefu alikuwa akitofautiana kauli na mama yake katika suala zima la uhusiano wake na Diamond lakini anamshukuru Mungu amemuelewa na sasa kila kitu kinakwenda sawa.
Staa wa filamu Bongo, Wema Sepetu akiwa na mama yake.
“Mama nilikuwa nikimsihi sana juu ya uchumba wangu na Diamond lakini sasa tumefikia hatua nzuri namshukuru Mungu amekubali, maana siku hizi nikionana naye ananiuliza vipi mwenzako mzima, anaendeleaje, wakati mwanzoni haikuwa hivyo,” alisema Wema huku akiahidi kumkutanisha Diamond na mama yake. Imeandikwa na Mayasa Mariwata na Shani Ramadhani

HABARI KAMILI ...»

TAARIFA EXCLUSIVE : HAMISA MOBETO KUVISHWA PETE YA UCHUMBA ... HABARI KAMILI SOMA HAPA

0 comments

Wanasema kimya kingi kina mshondo baada ya kudaiwa, hapo mwanzo ilidaiwa kua  Hamisa Mobeto alikua akichepuka na Bwana Almas aka Dangote aka Diamond au Chibu kama mwenyewe anavyopenda kujiita. Lakini baada ikaja kujulikana kua yalikua ni maneno ya wabongo.

Habari za kuaminika Bongoclan ilizozipata ni kua kwa sasa Mwanadada Hamisa kazama kabisa kwenye penzi zito la Seth De Jesus Giovan almaarufu kama Bikira wa kisukuma. Mmoja wa mashostito wa wapenzi hao ambaye hakupenda jina lake litajwe alisema kua Hamisa keshatambulishwa nyumbani kwao na Bikira na kilichobaki ni tukio la kuvishana pete ndo lililobakia.
Team yetu iliamua kufatilia kama ni kuna ukweli  kuhusiana na ishu ya kuvishana pete kwa wapenzi hao na kugundua ni kweli kua watavishana pete tarehe 2 ya mwezi wa 8 ndani ya Escape 1 ambako pia ndani ya siku hiyo kutakua na Instagram Party.



Kupitia akaunti yake bikira wa kisukuma alifunguka haya kuhusiana na tukio hilo " Mungu anipe nini mie...Nimeokota Embe Dodo vhini ya Mpera..I cant wait tarehe 2 pale ESCAPE 1.. Asante Mungu kwa kuileta INSTAGRAM maana nisingempata huyu na kudolishia watu hapa... Nakupenda we mtoto kuliko Ng'ombe anavyopenda majani,Nakuhusudu kuliko Mngoni anavyopenda ngono,Nakuthamini kama Mchungaji anavyoithamini Biblia... I cant wait to engage you pale jukwaani mbele ya halaiki maelfu TAREHE 2...Kama Chibu kaweza kwanini mie nishindwe...Niko tayari kuwa bwege juu yako hamisa wangu,Sitakuwa na wivu wala SitakuSPY kama mme wa yule dada nanii yule mtangazaji,Msukuma nimezama kwako @hamisamobeto DONT MISS MY ENGAGEMENT PARTY kwenye INSTAGRAM PARTY TAREHE 2...iam excited..Nikipigwa kibuti ntalia balaa ntafunga akaunti wallah"
 
Pia inadaiwa kua Hamisa amewaalika mastar mbalimbali ambao watahudhuria tukio hilo wakiwemo Diamond akisindikizwa na Wema,  Adam Mchomvu, William Malecela, Jerry Slaa na wengine kibao huku burudani ikitolewa na Skylight Band.
Kiingili siku hiyo itakua ni elfu 10 tu huku mambo yakianza mapema kuanzia saa1 ya usiku.
Unakaribishwa Kusoma habari za udaku na za siasa kila siku, usikubali kupitwa, like page yetu ya swahilitz katika facebook na pia usisahau kutufollow katika instagra @swahilitz vile vile katika twitter @swahilitz1. unakaribishwa kutoa maoni yako hapo chini.

HABARI KAMILI ...»

RAIS WA BARACK OBAMA ANUSURIKA KUBURUZWA MAHAKAMANI.

0 comments

 US President Barack Obama, pictured in Honolulu, Hawaii, on December 23, 2012 (AFP_File, Jim Watson) Rais Barack Obama wa Marekani.


Baraza la Wawakilishi la bunge la Marekani linaloongozwa na chama cha Republican lapiga kura Jumatano kumshtaki Rais Barack Obama kwa madai ya kukiuka madaraka yake ya kikatiba.

Baraza hilo limepiga kura 225 dhidi ya 201 kuunga mkono hatua hiyo isio na kifani ya kumburuza rais mahakamani kwa kutotii sheria ipasavyo wakati akiutekeleza muswada wake wa marekebisho ya huduma za afya unaojulikana kama "Obamacare"

Hatua hiyo itamwezesha spika wa baraza hilo la wawakilishi la bunge la Marekani John Boehner kuanza kushughulikia taratibu za kisheria za kumdhibiti rais ambaye amesema amelewa madaraka.

Boehner amesema suala hilo halihusu mvutano kuhusu wabunge wa chama tawala cha Demokrat au Republican bali ni suala la kutetea katiba na kuchukuwa hatua madhubuti wakati katiba hiyo inapohatarishwa.

Kutetea katiba

John Boehner Spika wa Baraza la Wawakilishi la Bunge la Marekani.

Amekaririwa akisema "Mko tayari kumuachia rais yoyote yule kuchaguwa sheria gani za kuzitekeleza na sheria gani za kuzibadilisha ? Mko tayari kumuachia yoyote yule kukivunjilia mbali kile kilichojengwa na waasisi wetu ? Msifikirie tu juu ya kiapo mlichokula bali fikirieni jinsi mlivyokula kiapo hicho mkiwa kama chombo kilichosimama pamoja.Hicho ni kitu pekee ninachowaomba leo hii kuitetea katiba kwa niaba ya wananchi tunaowatumikia."

Boehner amewaambia wabunge wenzake kwamba Obama amekiuka katiba mama ya nchi hiyo kwa kutofuata kikamilifu tafsiri ya kisheria wakati wa kutekeleza marekebisho ya sheria ya afya.

Kwa upande wake Rais Obama amepuuzilia mbali kwa kuikejeli hatua hiyo ya kutaka kumfungulia mashtaka wakati akizungumza kwenye hotuba aliyoitowa huko Kansas City katika jimbo la Missourri.

Amesema huku akishangiliwa na umma uliokuwa ukimsikiliza na kwamba "Badala ya kunishtaki kwa kufanya kazi yangu vizuri, nalitaka bunge kufanya kazi yake kuboresha zaidi maisha ya Wamarekani ambao ndio waliowapeleka bungeni."

Obama pia amewakumbusha wananchi kwamba kwa vyoyote itakavyokuwa ni wao ndio wataobebeshwa gharama za kulipia kesi hiyo mahakamani.

Demokrat yalaani hatua hiyo

Wabunge wa chama cha Demokrat nao hawakupoteza wakati kuilani kura hiyo ya kumfungulia mashtaka rais.

Mbunge mwandamizi wa Demokrat Nancy Pelosi naye ameghadhibishwa na hatua hiyo ya kwanza ya kumshtaki rais katika historia ya Marekani na kumlinganisha na mtu dalimu.

Nancy Pelosi kiongozi wa wabunge wa Demokrat katika Baraza la Wawaklishi la bunge la Marekani.
Amesema inatia kichefu chefu, ni siasa chafu na kutomheshimu kabisa rais.

Debbie Wasermann Schultz mbunge wa chama hicho kwa jimbo la Florida amesema ni jambo lisilo na tafakuri kwamba wabunge wa Republican baada ya kukosa cha kufanya hatimae wameamuwa kufanya kitu kumshtaki rais kwa kufanya kazi yake wakati wakigoma kufanya yao.

Ameongeza kusema laiti angeliweza kusema hiyo ni siasa chafu kuwahi kuishuhudia na amewataka wapinzani na wabunge wa Republican wasipoteze fedha za walipa kodi kwa azimio hilo na badala yake waungane na wenzao wa Demokrat kushughulikia changamoto nzito zinazoikabili nchi yao.

HABARI KAMILI ...»

WALIOKUFA AJALI YA DODOMA WAONGEZEKA,DEREVA ALIKUWA ANAONYESHA MWANAFUNZI HAWEZI KUMPITA

0 comments


IDADI ya watu waliokufa katika ajali ya Dodoma imeongezeka baada ya mtu mwingine kufa .
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi David Misime amesema tukio hilo la Pandambili Wilayani Kongwa katika barabara ya Dodoma – Morogoro limesababisha vifo vya watu 18 wanaume watu wazima 11 na mtoto mmoja wa kiume na Wanawake watu wazima 5 na mtoto 1 wa kike.
 Majina ya Marehemu hao ambao wametambuliwa na ndugu zao na kusafirishwa kwenda makwao kwa maziko ni:-
 1.   Christina d/o Dickson, Miaka 35, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Mpwapwa
 2.   Omari s/o Mkubwa, Miaka 32, Muhaya, Kondakta wa bus, Mkazi wa Morogoro
 3.   Malick s/o Masawe, Miaka 42, Mfanyabiashara, Mkazi wa Mpwapwa
 4.   Wilson s/o Paul @ Suda, Miaka 63, Mgogo, Mstaafu  Red Cross, Mkazi wa Mpwapwa.
 5.   Said s/o Lusogo, Miaka 44, mluguru, dereva wa bus, Mkazi wa Kihonda Morogoro.
 6.   Gabriel s/o Meja @ Chiwipe, Miaka 50, Mgogo, Mkazi wa Mpwapwa
 7.   Gilbert s/o Lemanya, Miaka 53, Mgogo, dereva wa Lori, Mkazi wa Makole Dodoma
 8.   Mikidadi s/o Zuberi @ Omari Miaka 22, Mbondei, Tingo wa Lori, Mkazi wa Morogoro/Ilala Dar es Salaam.
9.   Justine s/o Makasi, Miaka 24, Mgogo, Mkulima wa Mpwapwa
10.       Alice d/o Masingisa, Miaka 24, Mgogo, Mkazi wa Mpwapwa
11.       Merina d/o Doto @ Marcel, Mgogo, Miaka wa Mji mpya  Mpwapwa
12.       Nasibu s/oSeif, Miaka 48, Mkazi wa Morogoro
13.       Nicholaus s/o Raymond Kileo Miaka 51, Mkazi wa Mpwapwa
14.       Stella d/o Mdako, Miaka 60, Mkazi wa Mpwapwa
15.       Erick s/o Lucas,Miaka 10, Mkazi wa Morogoro
16.       Nazaret s/o Deremsi @ Kasuga, Miaka 45, Mhehe,  Mfanyabiashara, Mkazi wa     Kibakwe Mpwapwa.
17.       DArini d/o Dickson, Miaka 2, Mgogo, Mkazi wa Mpwapwa
18.       Magreth d/o Nyanzi, Miaka 35, Mgogo, Mfanyabiashara, Mkazi    wa Mwananyamala Dar es Salaam.
         Aidha majeruhi waliokuwa wanaendelea na matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kongwa wametibiwa na kuruhusiwa na wengine kuhamishiwa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Dodoma.
Waliobaki katika Hospitali ya Mkoa wakiendelea na matibabu ni 32 na wanaendelea vizuri isipokuwa walio katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu wa madaktari (ICU)  ambao ni George s/o Mjelwa, Miaka 40, Daktari wa Wilaya ya Mpwapwa na mke wake aitwaye Getrudar s/o Kombe, Miaka 37, Mfamasia wa Hospitali ya Wilaya ya Kondoa.
Jana kamanda alisema ajali hiyo baada ya uchunguzi zaidi inaonyesha kusababishwa na madereva wote wawili kwa maana ya dereva aliyekuwa anaendesha lori namba T 820 CKU/T390 CKT GILBERT S/O LEMANYA kwa kupita gari lingine bila kuwa mwangalifu na magari yaliyokuwa yanatokea mbele yake na kuwa katika mwendo kasi.
Dereva wa bus namba T 858 AUH SAID S/O LUSOGO kulingana na mashuhuda hasa abiria wanaeleza alikuwa mwendo kasi na ndiyo maana ajali hii imeleta madhara makubwa kiasi hicho kwani kama angelikuwa kwenye mwendo wa kawaida unaotakiwa madhara yangekuwa siyo makubwa kiasi hicho pamoja na dereva wa lori kufanya aliyofanya.
Wito kwa madereva na watumia barabara wengine waache mwendo kasi na ushabiki wa ushindani kwani kulingana na ushahidi uliokusanywa unaonyesha dereva wa Moro best alikuwa akiendesha kwa mwendo kasi kutaka kwenda kulipita bus la AL-SAEDY lililokuwa limeondoka mbele yake kwa kigezo kuwa dereva wa bus hilo ni mwanafunzi wake hivyo hawezi kufika Morogoro kabla yake.
Wamiliki wa Ma bus na magari mengine wawaonye madereva wao kuhusiana na mwendo kasi na kuwataka wazingatie sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali mbaya kama hii.
 Aidha abiria wasiwe wanakaa kimya kama walivyofanya wa bus la Moro best wanapoona dereva anaendesha kwa mwendao wa kasi watoe taarifa Polisi ili wakamatwe na kuepusha madhara kama yaliyotokea. 

Imetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.

HABARI KAMILI ...»

VIONGOZI WA UMOJA WA KATIBA YA WANANCHI (UKAWA)WATOA TAMKO LA LAO KUHUSU WITO ULIOTOLEWA NA VIONGOZI WA DINI KUWATAKA WAREJEE BUNGENI

0 comments



Viongozi wakuu wa Umija wa katiba ya wananchi (UKAWA) wakishikana mikono kuashiria umoja mara baada ya kuongea na wandishi wa habari kutoa Tamko la Ukawa kuhusu Wito wa Viongozi wa Dini wa kurudi Bungeni kutoka kulia ni profesa Sfari katibu mkuu wa NCCR mageuzi Mosena Nyambabe ,mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe ,Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba,Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi Jaqmes Mbatia na katibu mkuu wa Chadema Wilbrod Slaa , mbunge sakaya na Itatiro wakiwa nje ya makao makuu ya cuf
viongozi wa ukawa kulia ni mwenykiti wa umoja wa katiba ya wananchi ukawa profes Ibrahim Lipumba na mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowewakitoka katika ofisi kuu ya cuf wakielekea katika chumba cha mkutano tayari kuongea na wandishi wa habari kuhusu tamko lao kuhusu viongozi wa dini kuwataka warejee bungeni

Mwenyekiti wa Umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) Profesa Ibrahim Lipumba (katika)akisisitiza jambo wakati akiongea na wandishi wa habar kutoa Tamko kuhusu Wito wa Viongozi wa Dini wa kurudi Bungeni kushoto ni mwenyekiti awa Chadema Freeman Mbowe na kulia ni Mwenyeti wa NCCR mageuzi James Mbatia

HABARI KAMILI ...»

ANGALIA PICHA ZAIDI AJALI YA BASI ILIYOUWA WATU 17

0 comments



Basi la  Morobest lenye na namba za usajili T 258AHV lilipopata jali ya kugongana uso kwa uso na Lori
  na kuua Watu 17 katika eneo la Pandambili Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma ,Basi  liliokuwa likitoka Mpwapwa kwendaDar es salaam


Basi la  Morobest lenye na namba za usajili T 258 AHV lilipopata jali ya kugongana uso kwa uso na Lori na kuua Watu 17 katika eneo la Pandambili
Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma ,Basi  liliokuwa likitoka Mpwapwa kwendaDar es salaam


Lori lenye namba za usajili T 820 CKU na tela yenye namba za usajili T
390 CKT liliokuwa likiendeshwa na Dereva wake Gilbart Lemanya na Tingo
wake Mikidadi Zubery Omary  ambao wote walifariki papo hapo
linavyoonekana baada ya kugongana uso kwa uso na basi la Morobest
katika eneo la Pandambili Wilayani Kongwa  Mkoani Dodoma na

HABARI KAMILI ...»

BREAKING NEWS: WATU ZAIDI YA 14 WAMEFARIKI PAPO HAPO LEO KATIKA AJALI YA BASI LA MORO BEST LIKITOKEA MPWAPWA KWENDA DAR

0 comments


 Baadhi ya Miili ya Marehemu muda mchache baada ya kupata ajali wakiwa wanangojea kupelekwa Hospitali.


 Baadhi ya wasamalia wema wakiwa wanaendelea kuokoa majeruhi na kuwaondoa waliofariki 
Hivi ndivyo basi lilivyo Haribika
Fuatilia hapa 

Picha na Dodoma yetu Blog

HABARI KAMILI ...»

ANGALIA PICHA MAPOKEZI YA DIAMOND LEO ASUBUHI YALIVYO KUWA AKITOKEA MAREKANI

0 comments




 


 







HABARI KAMILI ...»

ALIYEDONDOSHA BOMU LA NYUKILIA HIROSHIMA AFARIKI DUNIA

0 comments


kapteni Theodore Van Kirk, katikati, na wenzake wakati wakirejea kutoka katika misheni ya Hiroshima, Japan Agosti 6, 1945. Kushoto kwake ni Kanali Paul Tibbetts kamanda wa msafara.
MWANAANGA wa mwisho katika  ndege aina ya B-29  (Enola Gay) iliyopiga mji wa Hiroshima uliopo Japan  na bomu la nyukilia (“Little Boy”) mji wa Hiroshima, amefariki dunia.Kwa mujibu wa The Atlanta Journal-Constitution,Mwanaanga huyo Theodore “Dutch” Van Kirk, 93, alikuwa navigeta  wa ndege hiyo ambayo Agosti 6 1945 ilidondosha bomu hilo na kumaliza vita vya dunia.
Van Kirk

Baada ya kifo cha   Morris Jeppson, mwaka 2010,Van Kirk alikuwa ndiye mpiganaji pekee aliyebaki kati ya wapiganaji dazeni walishiriki katika misheni hiyo.
Kwa miaka mingi alikuwa akiishi katika makazi ya wastaafu  huko Stone Mountain na walikuwa akiishi na James Starnes,  navigeta wa USS Missouri ambaye alipokea ujumbe wa kujisalimisha rasmi kwa Japan, Septemba 2, 1945.
Starnes, amesema rafiki yake alikufa Jumatatu baada ya kuwa hospitalini kwa wiki kadhaa.
Alisema kwamba kwa mara ya kwanza kwa miaka mingi alidondosha chozi kwa rafiki yake huyo ambaye kwa pamoja kwa nyakati tofauti walikuwepo wakati wa kuandika historia ya dunia.

HABARI KAMILI ...»

MSANII MWINGINE KUTOKA TANZANIA AKAMATWA NCHINI CHINA

0 comments


Mrembo almaarufu kwa jina la 'Winnie Mandela' katika muziki wa kizazi kipya akiwa amenaswa na polisi China.

HUKU modo maarufu Bongo, Jacqueline Fitzpatrick Cliff ‘Jack Patrick’, akisota jela nchini China kwa skendo ya kukamatwa na madawa ya kulevya (unga), mrembo mwingine ambaye aliwahi kujaribu kuchomoka kisanii kwenye muziki wa Kizazi Kipya almaarufu kwa jina la Winnie Mandela, naye amenaswa na polisi nchini humo.

Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kupitishwa kwa msako maalum wa kutokomeza biashara hiyo katika viunga vya Mji wa Hong Kong, China. 
JUX, PETIT MAN WAPATA WAKATI MGUMU
Kwa mujibu wa chanzo chetu chenye maskani yake Hong Kong, Mbongo Fleva, Juma Khaleed ‘Jux Vuitton’ na meneja wa msanii wa Bongo Fleva aitwaye Mirrow, Petit Man nao walijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kunusurika kuunganishwa kwenye oparesheni hiyo ya ukamataji wa waingizaji wa madawa ya kulevya nchini China.
'Winnie Mandela' wa muziki wa kizazi kipya Bongo akiwa chini ya ulinzi mkali China.

MADAI YA KUBEBA UNGA

Ilidaiwa kwamba Winnie alijikuta mikononi mwa askari wa China akidaiwa kubeba mzigo wa unga tumboni hivyo kukamatwa na kutembezwa mitaani kuelekea kituo cha polisi. 
APITA VIZUIZI, AKAMATWA
Ilisemekana kwamba Winnie ambaye ni msichana wa mjini Dar, alifanikiwa kupita vizuizi vyote lakini kwa hali ilivyo kwa sasa nchini humo ndipo akajikuta akikamatwa na kutembezwa mtaani kama mhalifu wa kivita. 
“Unaambiwa ilikuwa kama vita kwani polisi wa China huwa wana silaha za kutisha sana. Unajua Winnie alikamatwa kwenye mitaa ambayo kuna Wabongo wengi hapa Hong Kong,” kilisema chanzo chetu kutoka Hong Kong. 
Ilidaiwa kwamba askari hao walipokea agizo maalum kutoka kwenye kitengo cha kudhibititi madawa ya kulevya nchini humo kwani kwa sasa nchi hiyo imechafuka kwa uingizwaji wa madawa ya kulevya, jambo ambalo limeifanya serikali ya China ifanye oparesheni kubwa ya kuhakikisha wanatokomeza wimbi hilo. 
KWA WABONGO CHINA
Chanzo chetu kilisema kwamba kwa sasa Wabongo wanaokwenda au wanaokaa China wanaishi kama digidigi kwani wamefikia hatua ya kutoonesha pasipoti  zao na hata wengine wanadiriki kukataa uraia wao kwa kuwa Wabongo ndiyo wanasakwa kwa wingi.
“Sasa hivi jamaa wakisikia huyo ni Mtanzania wanamfuatilia sana kwani ndiyo wenye sifa ya uingizaji wa dawa za kulevya nchini China,” kilisema chanzo hicho na kuongeza: 

KAMA HUAMINI MUULIZE JUX AU PETIT MAN
“Hicho ndicho kilichomtokea Winnie. Nakwambia Wabongo wanazidi kukamatwa na madawa ya kulevya. Yaani ni aibu, huwezi kuamini.
“Wabongo wengi sana wamekamatwa Hong Kong na wengine familia zao Bongo hazijui.
“Kama Watanzania hawaamini wawaulize Jux na Petit Man ambao walishuhudia mtiti mwanzo mwisho.” 
BALOZI WA TANZANIA CHINA
Ili kupata undani na idadi ya Watanzania wanaokamatwa kwa ishu za madawa ya kulevya nchini China, gazeti hili lilimtafuta Balozi wa Tanzania China, Luteni General Abraham Shimbo ambapo simu yake ya ofisini iliita bila kupokelewa. Wakati Jack Patrick akisubiri kupandishwa kizimbani kwa mara nyingine mwezi ujao, ripoti zinaonesha kwamba wapo Watanzania wengi waliofungwa na wengine kunyongwa kwa msala wa madawa ya kulevya.

HABARI KAMILI ...»

HUYU HAPA NDIYO MTU MWENYE AKILI ZAIDI KULIKO WOTE DUNIANI

0 comments


Terrence Tao, He is a mathematician of Australian and American roots. If you think that math is hard enough, just take a peek into the subfields that Tao is involved with: additive combinatorics, analytic number theory, ergodic Ramsey theory, harmonic analysis, partial differential equations and random matrix theory.
A recipient of the Fields medal in 2006, Tao holds the James and Carol Collins chair in mathematics at the University of California, Los Angeles. He has had good training, learning math when he was barely a toddler, solving arithmetic problems at two years old, studying college level math at nine and getting a gold medal in the international math Olympiad when he was 13. He got his PhD when he was only 20 from Princeton and became a full professor at UCLA when he was 24. He has already published 230 research papers.

HABARI KAMILI ...»
Copyright © 2013. MSANGIBIN ALLY - All Rights Reserved
Customized by: MSANGIYUSUPHALY | Powered by: KIINICHAHABARI
Designed by: http://kiinichahabaribongo1.blogspot.com/