KUWA NA SHAHADA HAIMAANISHI MAISHA YATAKUWA MAZURI


Inawezekana umeshangazwa na kichwa cha habari, hata mimi ninashangaa kwanini nimefikiria hivyo. Baada ya kufikiria kuhusu elimu na maisha mazuri nikakumbuka kitu kimoja kutoka kwa mwandishi mmoja hivi, alisema kuwa “Elimu ni ufunguo wa maisha”. Suala ni kwamba kuwa na ufunguo umamaliza kila kitu, bali unaweza kuwa na ufunguo usijue ni wakufungulia wapi au nyumba gani. Je wewe una ufunguo wa maisha?
Ukija kwenye mfumo wetu wa elimu ni wa kukuelimisha au kukufanya ujue habari ya vitu fulani katika historia yetu na Lugha yetu na taaluma mbalimbali. Lakini ni mara ngani tumekuwa na wasomi wasiokuwa na mwelekeo wa maisha? Tunao wengi na wengine ni ndugu zetu, Hivyo elimu yao ni ufunguo wa maisha au kufuri la maisha?
Ninachotaka kukigusia ni kwamba elimu ya darasani sio pekee itakayokusaidia kuishi maisha ya huku mtaani, unahitaji elimu ya mazingira yanayokuzunguka. Shahada yako ni nyenzo tu ya kukuvuta na kukuweka kwenye fulsa fulani ila unahitaji ujuzi wa ziada katika kuishi maisha yanayostahili.

Usishangae kuona watu ambao wanaongoza kwa kuomba rushwa ni hao hao tunaosema wana elimu nzuri, tatizo ni nini? Watu wa elimu ya kati ndio wamekuwa wakimiliki uchumi kwa sehemu kubwa, kwakuwa wao hawaishi kutumia cheti, wanaishi kwa kutumia ujuzi walionao kufanya vitu wanavyofanya na hata kufanikiwa kuliko watu waliokwenda shule. Maisha mazuri ni mchanganyiko wa vitu vingi pamoja na elimu ya darasani , elimu ya mazingira yanayokuzunguka na ujuzi wa maisha kutoka vizazi vilivyopita.
Je wajua watu wanaomiliki makampuni makubwa ambayo inawezekana na wewe umeajiriwa huko, hawana elimu kubwa kuliko unavyofikiri ila wamekuajiri wewe wenye elimu uwatumikie? Je siri ni nini? Tafakari na uchukue hatua.
Kuwa na shahada inakupa fursa au upenyo wa kuingia sehemu fulani. Kama shahada inakupa upenyo wa kuingia au kukubalika sehemu fulani ila maisha mazuri yatategmea jinsi gani unavyotumia elimu ya darasani na ile ya mazingira yanayokuzunguka kufanyikisha malengo ya maisha yako.
Hivyo unapotumia elimu yako na kufanya kitu au mambo sahihi mafanikio yako sahihi yanaonekana, na vile vile unapotumia elimu yako kufanya mambo ambayo si sahihi utapata mafanikio ambayo si sahihi kwakuwa kuna kitu kimejificha kwenye mafanikio yako. Suala linakuja hivi je Kizazi kijacho kitaweza kuendeleza hayo mafanikio?

0 comments:

Copyright © 2013. MSANGIBIN ALLY - All Rights Reserved
Customized by: MSANGIYUSUPHALY | Powered by: KIINICHAHABARI
Designed by: http://kiinichahabaribongo1.blogspot.com/