RAIS WA BOLIVIA ‘EVO MORALES’ ASAJILIWA KUCHEZA SOKA LA KULIPWA



Rais Evo Morlaes
Rais wa serekali ya Bolivia ‘Evo Morales’ amekubali kusajiliwa na timu ya Sport Boys ya ndani ya nchi hiyo na kucheza soka la kulipwa.
Morales, mwanasoka wa siku nyingi amekubali kusajiliwa na klabu ya Sports Boys ya nchini mwake kwa ajili ya msimu ujao wa soka. Morales amesajiliwa na klabu hiyo yenye makazi yake katika Jimbo la Kusini Mashariki mwa nchi la Santa Cruz. Klabu hiyo imesema kwamba Rais Morales atakuwa akicheza walau dakika 20 kwenye mechi, kutokana na kazi zake nyingi za kuongoza nchi.
Morales (54) atakuwa akilipwa kima cha chini cha mshahara cha pauni 127 na klabu hiyo ya daraja la kwanza.
“Anapenda soka na pia anaweza kucheza vizuri, atavaa jezi namba 10. Tutamtumia orodha ya mechi zetu na yeye atachagua zile ambazo atapata nafasi,” akasema Rais wa Klabu ya Sport Boys, Mario Cronenbold.
Source:BBC

0 comments:

Copyright © 2013. MSANGIBIN ALLY - All Rights Reserved
Customized by: MSANGIYUSUPHALY | Powered by: KIINICHAHABARI
Designed by: http://kiinichahabaribongo1.blogspot.com/