Waislamu waaswa kutenda matendo mema hata baada ya Ramadhan
Waumini wa Dini ya Kiislamuwakifuatilia mawaidha.
Na MOblog Team
Waumini
wa Kiislamu nchini wamehaswa kuzingatia maadili kwa kufanya matendo
mema katika jamii, kwa kipindi chote watakachokuwa kwenye funga ya
Mwezi Mtukufu wa Ramadhan na baada ya kuisha kwa mwezi huo.
Akitoa
mawaidha hayo jijini Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa swala ya
Ijumaa wiki ya kwanza ya mfungo mwaka huu, Imam wa Msikiti wa Mtambani
Suleiman Abdallah alisema , Uislam ni dini ya amani hivyo ili mja aweze
kuwa karibu na Muumba wake anatakiwa kuzidisha ibada na kufanya mambo
yaliyo mema hasa kwenye mwezi wa Ramadhani.“Mwezi
huu sio mrefu, tumeweza kufanya mambo yetu kwa kipindi chote kwanini
tusivumilie katika nyakati fupi ambayo inamfanya mja kuwa daraja la juu
kiimani, inatakiwa kuyakimbia mambo ya kipuuzi yasiyokuwa na faida mbele
ya Allah, kwa kufanya ibada na kutekeleza funga kama inavyotakiwa,
tunatakiwa kuzidisha ibada, tuwe na subira, utiifu, nidhamu pamoja na
kuzidisha imani yetu kwa muda wote”
Imamu
alieleza kuwa, watu wengi wamekuwa wakivutiwa na mambo yanayopoteza
wakati na yasiyo na mazingatio wala manufaa katika maisha yao, hali ya
kuwa wakiacha kufanya matendo mema yanayompendeza Mwenyezi Mungu.
“Kuna
mazingatio makubwa yanayopatikana ndani ya Mwezi Mtukufu, kama kuongeza
imani zetu na kupata faradhi mbalimbali zitakazoongeza swawabu kwa
matendo tunayoyafanya, pia kuna tahadhari kwa waislamu tunakiwa
kuepukana nayo kama kuchanganya ibada na mambo yasiyokuwa na faida kama
kufuatilia mpira na mambo mengine yanayoweza kuaribu funga zetu wakati
tukiwa na swaum”.
Aliongezea
kuwa “Watu wanatakiwa kujikita zaidi kwenye ibada, kwani tunafunga
mwezi kwa mwaka tena ni siku chache hivyo watu wanatakiwa kuwa
wavumilivu ni kipindi kifupi cha mpito, lakini utakuta watu wanaingia
uvivu hatimaye mwezi unaisha bila ya kufanya ibada zozote muhimu”
0 comments: