VIWANGO VYA WACHEZAJI: ANGEL di MARIA NDIYE NYOTA WA MCHEZO WA FAINALI YA UEFA REAL IKITWAA `NDOO` YA 10, SHUKURANI KWA BAO LA BALE DAKIKA ZA NYONGEZA


La Decima: Real Madrid lifting their 10th European Cup

BAADA ya Real Madrid kufanikiwa kutwaa `ndoo` ya 10 ya UEFA kwa kuwafunga watani zao za jadi, Atletico Madrid katika kipindi cha dakika za nyongeza, mtandao huu unajaribu kukupa viwango vya wachezaji wote hapo jana na alama zinazotolewa kwa kila mchezaji ni 10. Diego Godin aliwafungia  Atletico bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza na kuukaribia ubingwa wa UEFA, lakini bao la kusawazisha la Sergio Ramos katika dakika za lala Salama  lilichafua hali ya hewa na kuulazimisha mchezo kuhamia dakika 120. Katika dakika hizo za nyongeza, Gareth Bale, Marcelo na Cristiano Ronaldo walipeleka machungu makubwa mno kwa Atletico waliobakiza mkia tu kutwaa `ndoo` .
 Viwango vya wachezaji wa Real Madrid:

Iker Casillas - Alifanya kosa kubwa na kufungwa bao la kwanza baada ya kutoka golini na kushindwa kuzuia mpira wa kichwa uliopigwa na Diego Godin. Alikuwa chini ya kiwango. Anapata alama 5
Daniel Carvajal - Alicheza vizuri na kuisaidia timu mara kadhaa. Anapata alama 6Raphael Varane - Alisimama imara kulinda lango lao na alihusika kuwachinja vijana wa Diego Simeone katika dakika za mwisho. Anapata alama 6.
Sergio Ramos - Alioneshwa kadi ya njano katika kipindi cha kwanza na mara nyingi alikuwa kama kachanganyikiwa mpaka alipofunga bao la kusawazisha kwa njia ya kichwa na kuwapeleka dakika za nyongeza. Anapata alama 7.
Fabio Coentrao - Alijituma sana, lakini alitolewa mapema kipindi cha pili. Anapata alama  5.Luka Modric - Alikuwa na kazi nyingi katika sehemu ya kiungo, lakini kiukweli alishindwa kuleta madhara kama alivyozoeleka. Anapata alama 6.

Rejoice: Iker Casillas and Marcelo celebrating their victory

Pivotal: Sergio Ramos scored the vital goal that got them back into the game

Sami Khedira - ilishangaza kumuona katika kikosi cha jana baada ya kukaa nje kwa muda mrefu kutokana na majeruhi ya goti na alitoa mchango wake kabla ya kutolewa. Anapata alama 6.
Angel Di Maria - Alikuwa bora kwa muda wote wa mchezo na ubora wake ndio uliobadilisha mchezo na kupata ushindi. Anapata alama 8. 

Gareth Bale - Alionekana kukosa umakini na kupoteza nafasi za kufunga na kuleta mashaka juu ya gharama kubwa iliyotumika katika usajili, lakini katika dakika za nyongeza alifunga bao muhimu mno, kama alivyofanya katika fainali ya Copa del Rey. Ananapa alama 6.

Cristiano Ronaldo - Alipiga vizuri mpira mmoja wa adhabu uliookolewa na mpira mmoja wa kichwa ambao haukulenga lango. Hakuwa fiti, japokuwa alifanya kazi nzuri dakika za mwisho na kuzalisha penati aliyofunga mwenyewe. Anapata alama 6.

Karim Benzema - Wakati wote wa mchezo hakuwa fiti kabisa. Anapata alama  5

Wachezaji wa akiba walioingia:
Isco - Alijaribu kuongeza nguvu kiasi. Anapata alama  6

Marcelo - Huyu ndiye aliyebadilisha mchezo kiuhalisia. Aliiongeza makali Real katika safu ya ushambuliaji na alifunga bao la tatu. Anapata alama 7.

Alvaro Morata - Aliingia dakika za mwisho za muda wa kawaida na alijitahidi kupambana. Anapata 6
Embrace: Pepe and Gareth Bale enjoying the post-match fesitivities
Safi jembe: Pepe na Gareth Bale wakishangilia wakati wa sherehe ya ubingwa baada ya mechi.

Specialist: Cristiano Ronaldo scoring the penalty that put them 4-1 up

Viwango vya wachezaji wa Atletico Madrid:

Thibaut Courtois - Alikuwa salama muda wote, aliokoa mipira michache na kuokota kwenye nyavu mpira mmjo wa Sergio Ramos katika dakika za kawaida. Na aliokota mipira nyavuni mara tatu katika dakika za nyongeza. Anapata alama 6.
Juanfran - Ni ngumu kumkosa beki yeyote wa Atletico. Dakika 30 za nyongeza zilikuwa nyingi sana kwake, lakini alipambana. Anapata alama 6

Miranda - Kwa mara nyingine, alifanya kazi kubwa mno. Anapata alama 6.
Diego Godin - Aliifungia Atletico bao la  kuongoza na bao lake la 6 msimu huu, ni wiki moja tu ambapo bao lake liliwapa ubingwa wa La Liga. Alifanya kazi kubwa na atakumbukwa daima. Anapataalama 7

Filipe Luis - Bale alimkimbiza sana, lakini alijitahidi kumzuia. Anapata alama 6

Raul Garcia - Alioneshwa kadi dakika za mwanzoni baada ya kumfanyia madhambi Di Maria, lakini hakukata tamaa. Mchezo ulibadilika baada ya kutolewa. Anapata alama  7
Dejected: Thibaut Courtois reacting to his side's defeat

Unhappy: Diego Simeone was unimpressed with the amount of stoppage time in the game

Tiago - Alikuwa na bahati kwasababu Bale hakuwaadhibu kwa makosa yake katika kipindi cha kwanza, lakini alifanya jitihada kubwa. Anapata alama 7.
Gabi - Alikuwa bora muda mwingi wa mchezo. Alitoa penati ya haki kabisa. Anapata alama  7.
Koke - Alicheza kwa nidhamu kubwa na kujitolea. Anapata alama 7

Diego Costa - Alianzishwa licha ya kuwa na majeruhi ya nyama za paja, na alicheza dakika 9 tu. Anapata alama 4.

David Villa - Alikimbiza mara kadhaa na kuwapa shida mabeki wa Real, lakini Atletico walishindwa kuendeleza kasi yao ya kushambulia na kumfanya asifanye kazi yake. Anapata alama 6

Wachezaji wa akiba walioingia:
Adrian: Aliingia dakika za mapema kipindi cha kwanza na alitoa mchango mkubwa. Anapata alama 7

Jose Sosa: Hakufanya kazi yake wakati alikuwa anahitajika sana. Lakini alijitahidi. Anapata alama 6.
Toby Alderweireld - Hakuweza kuwazuia Real dakika za nyongeza. Anapata alama 5 .
Fighter: Koke battling for the ball against Alvaro Morata

Hobble: Injured Diego Costa leaving the pitch after just nine minutes

ANCELOTTI KOCHA WA PILI KUTWAA `NDOO` YA UEFA MARA TATU, AWAPIGIA `SALUTI` WACHEZAJI WAKE KWA KUMWANDIKIA HISTORIA SAFI

Elevated: Carlo Ancelotti has become just the second manager in history to win three European Cups

Winner: Ancelotti also won the Champions twice with AC Milan in 2003 and 2007

0 comments:

Copyright © 2013. MSANGIBIN ALLY - All Rights Reserved
Customized by: MSANGIYUSUPHALY | Powered by: KIINICHAHABARI
Designed by: http://kiinichahabaribongo1.blogspot.com/