UKATILI!! BABA AUA MTOTO WAKE WA MIAKA MITATU KWA KIPIGO,KISA NI MKOROFI HAMSIKILIZI BABA YAKE


Kamanda wa polisi mkoa wa Geita-Joseph Konyo
Ukatili dhidi ya watoto umeendelea kutokea katika jamii ambapo mtoto James Wilson(3)mkazi wa kijiji cha Misri kata ya Bugalama wilayani Geita mkoabi Geita ameuawa kwa kupigwa baba yake mzazi kwa madai kuwa mtoto huyo amekuwa hamsikilizi baba yake kwa sababu ya ukorofi.

Akizungumzia tukio hilo diwani wa kata ya 
Bugalama Samweli william amesema baba mzazi wa mtoto huyo Wilson Chimba(46) alimtuma mtoto kununua mafuta alipokataa akaanza kumpiga.

Kufuatia kipigo hicho mtoto huyo alikwenda kujificha kwa jirani yake na siku iliyofuata baba mzazi alipomfuata mtoto huyo kisha kumpiga hadi kumuua.

 Jeshi la polisi mkoani Geita limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba tayari limemkamata mtuhumiwa huyo kwa kitendo hicho cha kinyama.

0 comments:

Copyright © 2013. MSANGIBIN ALLY - All Rights Reserved
Customized by: MSANGIYUSUPHALY | Powered by: KIINICHAHABARI
Designed by: http://kiinichahabaribongo1.blogspot.com/