BAADA KIMYA CHA MUDA MREFU MISS TANZANIA HAPENESS WATIMANYWA AIBUKA NA KUNENA MZITO
Miss Tanzania 2013, Hapiness Watimanywa, ameibuka na kusema kuwa kunyakuwa taji la urembo wa Miss Tanzania sio tiketi ya kuwa na skendo mbalimbali au kufanya mambo ambayo ni kinyume na maadili.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Happy alisema kuwa anaamini siyo kwamba mtu anapopata taji la urembo ndiyo linampa kichwa cha kuwa mcharuko, bali inategemea na uelewa wa mtu na mtu.
Mrembo huyo akaongeza kuwa, kwa upande wake anaamini atamaliza mwaka wake wa urembo akiwa ni msafi na wanaosubiria ang’are kwa skendo watasubiri sana.
0 comments: