ZIFAHAMU SABABU ZA RIDHIWANI KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA CHALINZE ... AWAPASHA WAGOMBEA WENZA
Ridhwani alisema hayo jana wakati
akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kurejesha fomu za
kugombea Ubunge wa jimbo hilo. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa
tiketi ya Chadema, Matayo Torongey, alinukuliwa akisema kuwa Ridhwani
hawezi kugombea Ubunge Chalinze kwa kuwa si mkazi wa jimbo hilo.
Katika mazungumzo yake na waandishi wa
habari, Ridhwani alionesha kushangazwa kuwa iweje akashifiwe kuwa yeye
si mkazi wa Chalinze.
“Yani (Torongey) anaweza kuniambia kuwa
mimi sio mkazi wa Chalinze? Hii inachekesha sana kwa kuwa kwanza ni nani
asiyejua kuwa mimi mzaliwa kabisa wa huku?” Alihoji Ridhwani.

0 comments: